Umeshonari Kibaigwa

USHUHUDA WA KIBAIGWA
Baada ya kumaliza huduma zanzimbar nilisikia sauti ya Bwana  ikiniambia kwenda Dodoma kwa wiki mbili mbele,nikampigia mchangaji GIDION mda huohuo,Akakubali na kutukaribisha kwa moyo wote,tukamsihi Bwana kutupa kibali cha kwenda na ndugu yangu wa thamani CHARLES,siku ya kwenda kulikuwa na vikwazo vingi sana hadi ndugu yangu akakwama moja kwa moja.
  Bwana akanipa kibali cha kwenda na nikafika salama siku ya ijumaa jioni tarehe 23/8/2013,kesho yake tukaanza mkutano wetu,ulikuwa ni mkutano ambao Bwana mwenyewe alikuwa kazini kwani nilimuona kwa dhahiri sana,
  Mchungaji mmoja wa kipentekoste  alikuja mkutanoni  na akasema nimekuja kujifunza na uchungaji wangu nimeacha pale nje,alikuja pamoja na baadhi ya washirika wake,  usingeweza kujua kuwa kulikuwa na wageni bali wote tulionekana  ni familia ya BRANHAM,kwa NENO  ambalo Roho alikuwa akileta pale kuanzia kwangu kama mhudumu nilipewa  palepale nami nikakituma kama lilivyo kwenye kusanyiko.
   Palikuwa na dada mmoja jina lake akiitwa Dada Mariam Chilongani (tazama picha)alikuja kwenye mkutano baada ya

 ndugu Peter ambaye alikuwa mchungaji wa kipentekoste pia amebatizwa  yeye na mke wake miezi michache iliyopita,alimwalika kuja kwenye mkutano, lakini kuna mama mmoja mke wa mchungaji  wa kanisa la kipentekoste,alimwambia kuwa hiyo imani wanaabudu vitu vya ajabu wana imani ya ajabu sana usiende kamwe,… Huku kukiwa na nguvu ya ajabu ikimwambia nenda.
   Hatimaye akafanikiwa kuja kwenye  mkutano huku akiwa amejaa wasiwasi mkubwa kwamba hawa watu  wanaamini ujinga,akiwa kwenye ibada anasema nilipoanza kuhubiri  alikuwa na dharau kubwa kuhusu,mimi yaani aliona kama ni kupoteza mda tu.
  Ghafra anasema”nilipokuwa naangalia nikaona muko wawili, na huyu wa pili anafunua KITABU na wewe unasoma na popote unapozunguka mimbarani upo pamoja naye,nikawa sielewi ni kweli naona mtu mwingine pale au? na ameenda saa ngapi mbona wote tumekaa? na wenzangu wanaona kama ninavyomuona?nikafikisha macho,bado naona muko wawili,na huyu wa pili amevaa kama wewe,mmefanana sana yaani kama naona taswira yako kwenye kioo. ila ameinama sikumuona sura yake lakini mlifanana,(THIOPHAN) na kila Ulichosema  alipokuonyesha pa kusoma kilichoma mimi  kile ninaishi katika maisha yangu niakaanza kuogopa maana naliona akikufuata kisha akatoweka ghafla huku nikioana kila kitu.”
    “Nikajua hapa huyu ni Mungu kabisa,endelea kuhubiri injili uko  na Roho mtakatifu kabisa popote unapokwenda nimemuona kwa macho yangu na anakutumia kweli usirudi nyuma songa mbele,na mimi sijabaki nilivyokuwa  najisikia amani sana moyoni kwani Mungu amenipa uhakika tofauti na nilivyoambiwa,naomba maombi sana ili Bwana anibadilishe nifanane naye,alisema dada …….”
  Namshukuru sana Bwana kwani dada alishuhudia kusanyiko la hapo na kila mmoja alibakia nashangaa na kuogopa.

Baada  ya siku kama tatu hivi huyu dada aliporudi kijijini kwake akawa anamshuhudia mama mmoja mambo aliyiyaona kwenye mkutano na kile sisi tunaamini, YULE MAMA  AKASEMA WAKO WAPI HAO WATU NIMEKUWA NAWATAFUTA MIAKA MINGI SANA TANGU NILIPOSIKIA TOKA KWA MHUBIRI MMOJA MOSES KULOLA MIAKA HIYO AKISEMA KUNA MJUMBE  ALIYE LETA NENO LA WAKATI WETU,ANAITWA BRANHAM,NILIPENDEZWA SANA NA HUO UJUMBE NIKATAMANI KUUJUA ZAIDI,..NIAMBIE WAKO WAPI NAENDA KUBATIZWA TANGU LEO MIMI SI MPENTEKOSTE TENA.
   Kijiji kizima kikawa kimesikia kile dada aliona na mke wa mchungaji alikokuwa dada anasali alikuja kumfuata na kumwambia imani gania hiyo? Ambayo hawaamini katika kunena kwa lugha,…akamwambia nimeshawishika na sasa ninahusika, ninamfuata nabii BRANHAM ambaye nina uhakika yuko mbinguni na siwezi kufuata wale ambao sina uhakika nao  wanafundisha uongo.
    Mama mmoja hapo kijijini alikuwa na tatizo la kutoka usaha mfululizo kwa zaidi ya mwaka mmoja,dada akamwambia mpigie ndg kambarage akuombee,huku akiwa ametembea hospitali nyingi pamoja na kuombewa katika madhehebu mbalimbali bila mafanikio, aliponipigia nikamwambia unaamini ?akasema ninaamini,nilikuwa ofisini,tukaomba kwa Bwana,naye Bwana akasikia akamponya,nilipompigia jioni ya siku hiyo, alikuwa na furaha ya ajabu asiamini kabisa kama shida yake imeisha,moto umeendelea hapo kijijini na familia ya Branhamu inaongezeka.tunaomba maombi yenu ili tusonge mbele kumtafuta kondoo wa mwisho kisha tuende kwa baba,AMEN
   Bro.kambarage

TANZANIA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni