Nilipo mpigia akashangaa sana kumbe
naye ananitafuta kwa mda mrefu,ndipo nikamwambia mchungaji tungependa kuja kuwatembelea kwa wiki mbili
zijazo,akasema haina shida karibuni sana,tukaomba kibali kwa Bwana, na akatupa tukafika
salama sana siku ya tarehe
9/8/2013,tukaanza mkutano jioni hiyo ya ijumaa,na siku iliyofuata
jumamosi na tukamalizia siku ya jumapili
tarehe 11/8/2013 ulikuwa ni mkutano wenye Baraka sana,na ambao ilikuwa ni ngumu
sana kuagana,..
Ilipofika siku ya jumatatu mchungaji
akasema tukawatembelee baadhi ya ndugu na dada ambao wapo mashambani tulienda na tukafika huko na kuwakuta ndugu
na dada ambao ni wa Baraka sana,wanaishi katikakati ya waislam,.kama ujuavyo Zanzibar
zaidi 95% ni waislamu tu,
Tulipokuwa kule Mchungaji alituambia kuwa
tuna paswa kuwa makini sana kwa sababu vile tulivyovaa tunajulikana kama ni
wakristo na hivyo wako makini sana kuangalia tunfanya nini,kwa sababu baadhi ya
ndugu walipigwa marufuku kushuhudaia huko na kuonekana huko.tulienda tukumkuta
ndugu na dada JOHN huko shambani katika nyumba ndogo na za nyasi kama unavyoona
kwenye picha hapo chini.walitukribisha kwa furaha sana moyoni lakini furaha yao
ilizuiwa na mazingira kwani alituomba kuwa tusiombe kwa mda mrefu kwani
tutakapoondoka tutamuachia matatizo makubwa nasi tulifanya hivyo ndani ya
dakika kumi tuliwaaga hawa bi arusi wa thamani wa kristo.
Baada ya hapo tulianza safari ya kumtembelea dada MONICA,tulimkuta yeye
na binti yake mdogo wakiwa katika kibanda kikukuu cha nyasi lakini wakiwa wenye
furaha sana,kama ujuavyo upendo wa kiungu ulioko katika familia ya Branham.Tulikaa
hapo kwa dakika kama kumi tukamtia moyo sana na kwa kweli ilikuwa ngumu sana
kuagana ndani ya dakika kumi wakati mnatamani kukaa zaidi ya siku mkiumega
mkate wa Bwana.
Tuianza safari ya kwenda mkoa mwingine tena shambani kumtembelea ndugu
Herman na wengine huko,tulifika salama na tukakuta ndugu amewakusanya baadhi ya
ndugu na dada,tukawa na ushirika wa neno kwa mda kama saa moja,na hawa watu
masikini wa shambani, Bwana akafanya njia kwao wakaamini ujumbe wa nabii
wetu,tukapanga kesho yake ya tarehe 12/8/2013 waje mjini tuwabatize
baharini,ilipofika siku hiyo waliwaambia na wenzao ambao hawakuwepo siku ya tukio
nao wakasema nasi tunaenda kubatiza,wakaja jumla yao nane tukawabatiza siku
hiyo,ilikuwa ni furaha iliyoje hapo baharini? Bwana anajua.
Huku zikiwa zimebaki kama dakika kumi ili boat iondoke kurudi Dar es
Salaam,ambayo ndio tulikataa tiketi zetu,tulimuomba Bwana kuwa afanye kama alivyofanya kwa nabii wetu
kusimamisha ndege kwa ajili ya bibi arusi mmoja aliye kuwa wa thamani machoni pa
Bwana, huku sisi tukiwa nao wanane.Bwana alijibu tulikuta haijaondoka,tulipopanda tukakumbatiana
kwa busu takatifu mimi na ndugu yangu wa thamani CHARLES,tukipongezana na huku
abiria wakituangalia wasijuea furaha yetu inatoka wapi.
Baada ya hapo Bwana aliendelea
kuwasha moto kwaani jumapili iliyofuata kanisa lilijaa na wengine wawili
wakabatizwa na mchungaji amekuwa na huduma ya kuwatembelea mara kwa mara kuwatia
moyo, na ili waje kanisani ina mlazimu kuwalipia nauli kwaani wengi wao ni
masikini mno.PIA KUMEKUWA NA BAADHI YA WAAMINIO WA SIRI AMBAO WAMEBATIZWA
LAKINI HAWAJAJITANGAZA WAZI KWANI WAKIFANYA HIVYO KUNA HATARI YA KUCHINJWA.
TUNAMUOMBA BWANA ATUPE KIBALI CHA KUFANYA MKUTANO MKUBWA SANA
ZANZIBAR MWEZI WA KUMI ILI BWANA AWEZE KUIBUA WENGINE HUKO KWAANI TUNAAMINI
WAPO,TUNAOMBA MOMBI YENU,MUOMBEE MCHUNGAJI KIMARO NA FAMILIA YAKE, NI NDG WA
BARAKA SANA WAMEJITOA KIKAMILIFU KUMTUMIKIA BWANA KATIKA MAZINGIRA HAYO MAGUMU.
BROTHER KAMBARAGE
TANZANIA
Picha za matukio zanzibar
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni